I made this widget at MyFlashFetish.com.

DarLeo

Usikubali kupitwa na Darleo kila siku jioni kwa Habari na matukio ya leo leo. Gazeti pekee la kila siku jioni. Sasa limesheheni habari moto moto kutoka mtaani kwako.

Thursday, September 9, 2010

Sababu za daladala kukatiza ruti zatajwa


Na Athman Hamza.

Kiwango cha nauli katika baadhi ya njia ndio sababu kubwa ya daladala kukatiza ruti Darleo limeelezwa. viango hivyo vidogo ukilinganisha na umbali wa safari huwalazimu madereva kuishia njiani au kuanza kupakia katikati ya ruti hususani maeneo ambayo abiria wakipanda hawashukii njiani.

Hayo yameelezwa na baadhi ya madereva wa daladala zifanyazo kazi yake kati ya Kawe na Buguruni wakati wakiongea na gazeti hili kuhusiana na sababu ya wao kuacha kupakia abiria mwanzo wa safari au kutangaza wanaishia njiani wakati wanaenda ampaka mwisho wa ruti.

Made reva hao wamesema kiwango cha nauli kikiwa kidogo na abiria kutaka kupanda mwanzo mpaka mwisho wa ruti inakuwa shida kupata hesabu ya siku hivyo kupelekea kuweka ajira zao hatiani.

"Ukiangalia ruti ya kawe buguruni na tabi ya abiria wa ruti hii utaona sababu ya sisi kusema tunaishia magomeni kwani abiria wakipanda hawashuki mpaka mwisho wa ruti" alisikikika dereva aliejitambulisha kwa jina la moja la Onesmo

Nae dereva Mrisho kasinde amesema bei ya nauli ya Buguruni Kawe na Buguruni- Msasani ni moja ya sababu inayofanya madereva kukatisha ruti na kuomba bei ya njia hizo kuangaliwa upya ili kuondoa tatizo hilo.
Abiria wa waendao Gongo la Mboto wakigombea kuindgia ndani ya daladala kutokana na adha ya usafiri nyakati za jioni kama walivyokutwa na mpiga picha wetu jana katika kituo cha basi cha Shule ya Uhuru.