Msomaji wetu kwanza tunakupongeza kwa kutumia hii blog hii kupata taarifa mbalimbali zinazoendelea jijini hususani zinazohusu Dala dala. Lengo la Blog hii ni kuishurutisha jamii ya watanzania ili kushinikiza maendeleo. Kwa kutumia Dala Dar Leo, usafiri Dar es salaam utabadilika na kuwa na mazingira mazuri kiasi cha kuruhusu watu wengi zaidi kuutumia. Hivyo tunaamni hili litakuwa ni jukwaa lako la kushiriki katika mijadala mbalimbali ili kuboresha huduma hiyo muhimu. Asante Mhariri
DarLeo
Usikubali kupitwa na Darleo kila siku jioni kwa Habari na matukio ya leo leo. Gazeti pekee la kila siku jioni. Sasa limesheheni habari moto moto kutoka mtaani kwako.
Wednesday, September 15, 2010
Serilkali yaombwa kuingilia kati ajira za madereva
Na Godfrey Ismaely, Jijini
SERIKALI imeombwa kuingilia kitendo cha baadhi ya wamiliki wa daladala kuwabadilisha wafanyakazi wao kila siku hivyo kuondoa umakini na kuwanyima haki walengwa.
Wito huo umetolewa kwa nyakati tofauti na wafanyakazi wa daladala zinazofanya safari zake kati ya Mnazi Mmoja na Tabata Segerea wakati wakizungumza na gazeti hili katika kituo cha Mnazi Mmoja kuhusu kutokuwa na mahusiano ya kutosha na matajiri wao.
"Sisi hapa tunabadilishwa kila siku kama nguo bwana, aheri serikali iweke mkazo kuhusu muda gani ambao tunatakiwa kudumu katika daladala moja kwani hata ile heshima inakuwa hamna tena licha ya kutunyima haki na kutufanya tukose umakini katika hii kazi," amesema dereva mmoja wa daladala aina ya DCM aliyejitambulisha kwa jina la Efferi Mohamed.
Ameongeza kuwa tangu aanze kufanya kazi ya udereva miaka miwili iliyopita amekuwa akiamishwa daladala baada ya daladala kwa madai kuwa hamna mtu mwenye hati miliki ya kukaa siku zote kuendesha daladala.
"Hata sisi hatupendi kuendesha daladala hizi ila tunalazimika kwa sababu hatuna jinsi, lakini inapofikia hatua mmiliki anakuambia kuwa mwenye "mandete" ya kutoa amri yeyote juu ya daladala husika na kukufukuza wakati ujajipanga huu ni unyanyasaji au unaambiwa una hati miliki hilo ndio suala gani tena," ameendela kusisitiza dereva huyo Mohamed.
Naye mfanyakazi mwingine wa daladala hizo aliyejitambulisha kwa jina moja la Lema amesema kuwa licha ya kuelezwa kila siku kuwa kuna mchakato wa kupatiwa mikataba ya ajira katika daladala zoezi hilo linaweza lisifanikiwe vyema.
"Kwanini niseme hivyo ni kwa sababu uwajibikaji hauonekani hivyo tunahitaji kwanza serikali ilitupie macho suala la kuhimiza mahusinao mazuri kati yetu na wamiliki wote wa daladala la si hivyo tutakuwa tunawapigia mbuzi gitaa," amesema Lema.
SERIKALI imeombwa kuingilia kitendo cha baadhi ya wamiliki wa daladala kuwabadilisha wafanyakazi wao kila siku hivyo kuondoa umakini na kuwanyima haki walengwa.
Wito huo umetolewa kwa nyakati tofauti na wafanyakazi wa daladala zinazofanya safari zake kati ya Mnazi Mmoja na Tabata Segerea wakati wakizungumza na gazeti hili katika kituo cha Mnazi Mmoja kuhusu kutokuwa na mahusiano ya kutosha na matajiri wao.
"Sisi hapa tunabadilishwa kila siku kama nguo bwana, aheri serikali iweke mkazo kuhusu muda gani ambao tunatakiwa kudumu katika daladala moja kwani hata ile heshima inakuwa hamna tena licha ya kutunyima haki na kutufanya tukose umakini katika hii kazi," amesema dereva mmoja wa daladala aina ya DCM aliyejitambulisha kwa jina la Efferi Mohamed.
Ameongeza kuwa tangu aanze kufanya kazi ya udereva miaka miwili iliyopita amekuwa akiamishwa daladala baada ya daladala kwa madai kuwa hamna mtu mwenye hati miliki ya kukaa siku zote kuendesha daladala.
"Hata sisi hatupendi kuendesha daladala hizi ila tunalazimika kwa sababu hatuna jinsi, lakini inapofikia hatua mmiliki anakuambia kuwa mwenye "mandete" ya kutoa amri yeyote juu ya daladala husika na kukufukuza wakati ujajipanga huu ni unyanyasaji au unaambiwa una hati miliki hilo ndio suala gani tena," ameendela kusisitiza dereva huyo Mohamed.
Naye mfanyakazi mwingine wa daladala hizo aliyejitambulisha kwa jina moja la Lema amesema kuwa licha ya kuelezwa kila siku kuwa kuna mchakato wa kupatiwa mikataba ya ajira katika daladala zoezi hilo linaweza lisifanikiwe vyema.
"Kwanini niseme hivyo ni kwa sababu uwajibikaji hauonekani hivyo tunahitaji kwanza serikali ilitupie macho suala la kuhimiza mahusinao mazuri kati yetu na wamiliki wote wa daladala la si hivyo tutakuwa tunawapigia mbuzi gitaa," amesema Lema.
Subscribe to:
Comments (Atom)
