Na Mwandishi Wetu, jijini
ASKARI wa Usalama Barabani wameombwa kuweka ulinzi mkali katika eneo la kituo cha Zakhem, Mbagala ili kupunguza kero ya foleni inayosababishwa na madereva kupakia abiria wakiwa wamesimama barabarani.
Wakizungumza na mwandishi wa gazeti hili kwa nyakati tofauti, baadhi ya abiria wamedai kuwa kutokana na kuwepo kwa kero hiyo, kumekuwa na foleni kubwa katika eneo hilo.
Wamedai kuwa baadhi ya madereva wamekuwa wakishindwa kufuata sheria na kusimama barabarani bila ya kujali usalama wa abiria.
"Eneo hilo hivi sasa limekuwa kero hasa nyakati za jioni na hiyo yote inatokana na madereva kuegesha magari yao barabarani huku wakipakia abiria na kusababisha gari la nyuma kushindwa kuendelea na safari, " amedai mkazi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Daud Hosea.
Amedai kuwa ili kuondokana na kero hiyo ni bora askari wakaongeza juhudi za kuweka ulinzi ili kuwabaini madereva hao wasiopenda kufuata sheria za usalama barabarani.
Naye Emmanuel Joakimu, mkazi wa Mbagala Kibonde Maji amedai kuwa kero hiyo pia imechangia kuwepo kwa baadhi ya madereva kukatisha ruti na kusababisha kuwepo kwa usafiri mgumu.
"Madereva wengine wanaamua kukatisha ruti kwani kitendo cha kufika hadi Mbagala Rangi Tatu inaweza ikamchukua saa moja ambapo umbali wake ni mdogo sana, " amedai mkazi huyo.
Mwandishi wa gazeti hili pia alishuhudia kuwepo kwa msongamano wa magari katika kituo hicho ingawa pia hali hiyo inachangiwa na ufinyu wa kituo cha Mbagala Mwisho na magari kushindwa kupishana.
Msomaji wetu kwanza tunakupongeza kwa kutumia hii blog hii kupata taarifa mbalimbali zinazoendelea jijini hususani zinazohusu Dala dala. Lengo la Blog hii ni kuishurutisha jamii ya watanzania ili kushinikiza maendeleo. Kwa kutumia Dala Dar Leo, usafiri Dar es salaam utabadilika na kuwa na mazingira mazuri kiasi cha kuruhusu watu wengi zaidi kuutumia. Hivyo tunaamni hili litakuwa ni jukwaa lako la kushiriki katika mijadala mbalimbali ili kuboresha huduma hiyo muhimu. Asante Mhariri
DarLeo
Usikubali kupitwa na Darleo kila siku jioni kwa Habari na matukio ya leo leo. Gazeti pekee la kila siku jioni. Sasa limesheheni habari moto moto kutoka mtaani kwako.
Friday, October 1, 2010
Madereva wapongeza polisi kuwapiga wenzao makofi
Na Stella Aron, Mombasa
BAADHI ya madereva wamewapongeza Askari wa Usalama Barabarani na wale wa kutuliza ghasia (FFU) kwa kuwaadhibu kwa kuwapiga makofi wenzao wanaokiuka sheria za barabarani
Madereva hao wanaoanza safari zao katikati ya jiji kuelekea Gongo la Mboto, wamepongeza adhabu hiyo inayofanywa papo kwa papo na askari hao waliopo kituo cha Mombasa.
Wakizungumza na Dar Leo kwa nyakati tofauti, baadhi ya madereva hao wamedai kuwa kutokana na kuanzishwa kwa adhabu hiyo, kumesaidia kupunguza kuwepo kwa madereva wanaopita pembeni wakati mwingine hata misongamano.
"Tunawapongeza askari hao kutokana na kuweza kukabiliana na madereva hao ambapo hivi sasa kero hiyo imepungua, " amedai dereva mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Hassan Omary, anayeendesha gari aina ya DCM kutoka Gongo la Mboto kwenda Kariakoo.
Kassim Swalehe, anayeendesha gari litokalo Gongo la Mboto kwenda Ubungo, hali kadhalika amepongeza adhabu hiyo inayotolewa na polisi.
"Kweli tunawashukuru hawa askari kwani ilikuwa kero kubwa sana ambayo ilikuwa ikisababishwa na sisi wenyewe, hata hivyo tunaomba tabia ya kuwachapa vibao madereva wasiopenda kufuata sheria za barabarani iendelee na hata kwa maeneo mengine, " amedai dereva huyo.
Hivi karibuni Kamanda wa Usalama Barabarani nchini , Mohamed Mpinga alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa foleni kwenye maeneo ya nje ya mji, vikosi mbalimbali vya usalama vimekuwa vikisaidia ili kupunguza kero hiyo.
BAADHI ya madereva wamewapongeza Askari wa Usalama Barabarani na wale wa kutuliza ghasia (FFU) kwa kuwaadhibu kwa kuwapiga makofi wenzao wanaokiuka sheria za barabarani
Madereva hao wanaoanza safari zao katikati ya jiji kuelekea Gongo la Mboto, wamepongeza adhabu hiyo inayofanywa papo kwa papo na askari hao waliopo kituo cha Mombasa.
Wakizungumza na Dar Leo kwa nyakati tofauti, baadhi ya madereva hao wamedai kuwa kutokana na kuanzishwa kwa adhabu hiyo, kumesaidia kupunguza kuwepo kwa madereva wanaopita pembeni wakati mwingine hata misongamano.
"Tunawapongeza askari hao kutokana na kuweza kukabiliana na madereva hao ambapo hivi sasa kero hiyo imepungua, " amedai dereva mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Hassan Omary, anayeendesha gari aina ya DCM kutoka Gongo la Mboto kwenda Kariakoo.
Kassim Swalehe, anayeendesha gari litokalo Gongo la Mboto kwenda Ubungo, hali kadhalika amepongeza adhabu hiyo inayotolewa na polisi.
"Kweli tunawashukuru hawa askari kwani ilikuwa kero kubwa sana ambayo ilikuwa ikisababishwa na sisi wenyewe, hata hivyo tunaomba tabia ya kuwachapa vibao madereva wasiopenda kufuata sheria za barabarani iendelee na hata kwa maeneo mengine, " amedai dereva huyo.
Hivi karibuni Kamanda wa Usalama Barabarani nchini , Mohamed Mpinga alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa foleni kwenye maeneo ya nje ya mji, vikosi mbalimbali vya usalama vimekuwa vikisaidia ili kupunguza kero hiyo.
Subscribe to:
Comments (Atom)